VITA YA VILABU: Yanga na Azam FC Waingia Kwenye Vita Kali Kunasa Saini ya Chobwedo
Soko la usajili limezidi kuchafuka nchini baada ya klabu za Yanga SC na Azam FC kuingia vitani vikali kuwania saini ya kiungo tegemeo wa TRA United, Ramadhani Chobwedo. Chobwedo amekuwa lulu sokoni kutokana na uwezo wake mkubwa aliouonesha msimu huu, jambo linalomfanya kila tajiri wa soka kutaka kuweka mzigo mezani.
Wakati Azam wakijinasibu kwa dau nono, Yanga wanatumia ushawishi wa kushiriki michuano mikubwa kama chambo cha kumnasa kiungo huyo. Mashabiki wanasubiri kuona ni wapi mchezaji huyo atatua huku akitajwa pia kuwa kwenye rada za Simba Sc.

Comments
Post a Comment
Maoni yako ni muhimu kwetu! Unafikiri nini kuhusu mchezo au tetesi hii ya leo? Shusha mchango wako hapa chini. Kumbuka: Lugha ya staha na heshima kwa wadau wote wa soka inazingatiwa.