🏟🎯SIMBA IPO KWENYE MAWINDO MAKALI YA KUMUNASA KIUNGO MSHAMBULIAJI RAIA WA NIGERIA🚨, IBRAHEEM JABAAR ⚽️

Klabu ya wekundu wa msimbazi SIMBA SC wanaoneka kudhamiria kuboresha katika safu ya kiungo mshambuliaji. Tetesi za ndani za michezo zinaeleze kuwa simba sc wameingia vitani kuwania saini ya mchezaji Raia wa Nigeria🇳🇬, IBRAHEEM JABAAR aliyekuwa ikiitumikia klabu ya stellenbosch Fc ya nchini Africa kusini.


Tetesi  hizi zimepamba moto baada ya klabu ya stellenbosch kutangaza kuachana na mchezaji huyo baada ya kumaliza mkataba nae na kuwa mchezaji huru, ambapo ibraheem jabaar ameitumikia timu hiyo kwa mda wa misimu mitano iliyopelekea kutwaa baadhi ya tuzo.

Rekodi za ibraheem jabaar akiwa kwenye timu ya stellenbosch 

1. Ameitumikia stellenbosch Fc kwa mda wa misimu mitano kuanzia February 2021 hadi June 2026
2.Amecheza mashindano ya kimataifa Caf confederation cup
3. Amecheza michezo 140 na kushinda tuzo ya mchezaji kijana kucheza michezo mingi kwenye timu hiyo

Mambo yanayopelekea kumfanya IBRAHEEM JABAAR kuwa mchezaji bora wa kipekee;

1. Mguu wake wa kushoto, jabaar anatumia silaha yake hiyo kwa kutengeneza pasi za mwisho, kutengeneza nafasi za magoli na kufunga pia.

2.Udhoefu wa soka, jabaar amecheze mashindano ya ushindani huko Africa kusini kwa misimu kalibia mitano na kuonesha ukomavu wa soka.

3. Mbinu yake ya uchezaji, jabaar ni mchezaji wa Kisasa na umri wake unaruhusu kufanya mambo makubwa uwanjani, anauwezo wa kuipatia timu yake ushindi.

SIMBA SC, Suala la viungo wabunifu limekuwa likiwapasua kichwa mashabiki wa Simba kwa muda mrefu. Kuja kwa mchezaji mwenye wasifu  kama ya Jabaar kunaweza kuongeza nguvu ya ushindani na kuwapa mashabiki burudani ya soka la pasi fupi na la haraka ambalo klabu hiyo inasifika nalo.

Huku dirisha la usajili likiwa bado linaendelea, macho yote ya wapenzi wa soka nchini yameelekezwa Msimbazi kuona kama dili hili litakamilika rasmi.

Je wewe kama  mashabiki damu damu wa weknudu wa msimbizi simba sc unahisi usajili huu utafanikiwa na jabaar ataleta matunda kwenye timu ya simba sc,? Shusha comment yako hapo chini 👇 👇👇




#SimbaSC #NguvuMoja #WekunduWaMsimbazi #TetesiZaUsajili #UsajiliTanzania #SokaLaBongo #HabariZaMichezo #LigiKuuYaNBC#SimbaKwanza #SimbaDay #SimbaTamuu #SimbaApp #Wanasimba #SimbaLeo

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA ALPHONCE MSANGA (MABULA) YA SOKA: Kutoka kwenye maisha ya mtaani hadi kuwa mchezaji bora wa kimataifa

Wasifu wa Albert Kangwanda Jr: Nyota Mpya wa Kimataifa Anayetamba Ndani ya Kikosi cha Yanga SC

Wachezaji bora kwenye ligi kuu ya NBC Premier League

RIPOTI KUTOKA KAMBINI: Uchambuzi wa Kikosi cha Taifa Stars na Silaha Mpya Kuelekea AFCON 2027

Fabrizio Romano Aitambulisha Yanga Duniani, Bodi ya Ligi Yaibeba Simba SC!

Rungu la TPLB: Maafisa wa Singida Black Stars Watandikwa Faini ya Tsh Milioni 20!

Mtanange wa Ligi Kuu ya NBC: Uchambuzi wa Kina wa Mechi za Kukata na Shoka Kesho

Mwelekeo wa Ligi Kuu ya NBC: Rejesho la Aziz Ki, Changamoto ya Majeraha Simba SC na Shinikizo Ndani ya Azam FC

WASIFU KAMILI: Fahamu Nguvu na Udhaifu wa Gaborone United, Wapinzani wa Yanga SC Ligi ya Mabingwa Afrika!

Ratiba Kamili na Utabiri wa Kimbinu wa Michezo ya Ufunguzi Ligi Kuu ya NBC Wikiendi Hii.