HISTORIA YA ALPHONCE MSANGA (MABULA) YA SOKA: Kutoka kwenye maisha ya mtaani hadi kuwa mchezaji bora wa kimataifa
ALPHONCE MSANGA (MABULA), ni miongono mwa viungo wanaotajwa kuwa na viwango wa kimataifa na wenye umri mdogo nchi Tanzania kw sasa. Maisha ya Awali na Soka la mtaani; Mabula alizaliwa na kukulia Tanzania kama walivyo vijana wengine, Alijiunga na soka la vijana wa mtaani akiwa na umri mdogo sana, alianza kucheza kiungo mkabaji, uwezo wake wa soka, utulivu, upigaji pasi sahihi na ukakamavu vilianza kuonekana kwenye mashindano ngazi ya shule na mitaani. Maisha na malezi ya Spartan academy (Spartan Boys); Mabula alijiunga na kituo cha mpira cha kulea na kukuza vipaji vya vijana kilichopo Dar Es Salaam. Hapa ndipo alipoanza kupata mafunzo na maisha ya soka, Spartan academy ikiwa na viwango bora vya makocha vilimpelekea Mabula kiwango chake kupanda kwa haraka na kuwa mchezaji mwenye kuaminika, hapa ndo alifundishwa namna ya kuusoma mchezo, namna ya kukaa kwenye eneo, namna ya ukabaji, na namna ya kujiamini akiwa uwanjani. Timu ya vijana ya soka Tanzania; Kwa kiwango alichoku...