UJIO MPYA WA SHEREHE YA KILELE CHA WIKI YA MWANANCHI (Yanga day).
Mashabiki wa Yanga sc, wanajangwani kaeni mkao wa kula maana msimu huu yanga sc imekuja kwa vingine tofauti na miaka mingine akisema Rais wa klabu yanga sc,Injinia Hersi Said "Kuelekea katika kilele cha mwananchi Yanga day, maandalizi ya sherehe hiyo teyari yameshakamilika kila kitu kwa idara zote".
Injinia Hersi Said alipokuwa kwenye mji wa Katoro-Geita kupitia taarifa ya habari ya azam Tv alizungumza maneno hayo siku ya ijumaa tarehe 24 mwezi huu na kuutaja mji wa Katoro ndiyo utakaotumika kwaajili ya wiki ya mwananchi na kufafanua ratiba na muongozo watakao kuwa nao Kuelekea yanga day;
1. Injinia Hersi Said, alitangaza mwisho wa mwezi huu kutakuwa na uzinduzi wa jezi zitakazotumika msimu wa 2026/2027.
2. Mkutano mkuu wa mwaka wa yanga sc utakaofanyika mwezi wa nane tarehe 2. (agosti 2, 2026).
3. Mwanza, matukio maalumu na uzinduzi wa yanga sc Kuelekea Yanga day utahamia kwenye Jiji hilo kati ya tarehe 3 au 4 mwezi. wa nane(agosti).
4. Tarehe 9 agosti, 2026 hii siku ndiyo itakakayokuwa hitimisho la sherehe za Yanga day, utambulisho wa wachezaji waliosajiliwa(maingizo mapya) na waliokuwepo, sherehe hiyo itafanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na kutakuwa na mechi ya kirafiki.
Malengo ya klabu ya Yanga sc msimu huu;
Maandalizi ya kuelekea msimu huu wa Ligi Kuu NBC, teyari Yanga sc washaanza kujiandaa na pre-season. Yanga sc msimu huu wanatarajia kuwa mabingwa tena kwa mara nyingine msimu huu 2026/2027, na nguvu zao nyingi hasa wamezielekezea kwenye mashindano makubwa ya ushindani hasa mashindano ya kimataifa, Ligi ya mabingwa Afrika (Caf Champions League).
Pia Yanga sc wamepania kubeba ndoo za ligi za ndani kama kombe la shirikisho (CRDB BANK Federation Cup, kombe la muungano pamoja na ngao ya jamii.

Comments
Post a Comment
Maoni yako ni muhimu kwetu! Unafikiri nini kuhusu mchezo au tetesi hii ya leo? Shusha mchango wako hapa chini. Kumbuka: Lugha ya staha na heshima kwa wadau wote wa soka inazingatiwa.