Simba SC Yapania Kuchukua Kila Kitu Msimu Ujao, Ahmed Ally Atuma Onyo kwa Wapinzani!
Mambo yameanza kupamba moto ndani ya kambi ya Simba SC kuelekea maandalizi ya msimu mpya. Kupitia kwa msemaji wake, Ahmed Ally, klabu hiyo imeweka bayana azma yake ya kutawala soka la bongo na kimataifa kwa kuchukua makombe yote yaliyo mbele yao.
Ahmed amesisitiza kuwa kipaumbele cha kwanza ni kurudisha heshima ya ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara na mashindano mengine yote yaliyo chini ya usimamizi wao msimu ujao.
Je, unafikiri Simba SC itafanikiwa kubeba makombe yote msimu ujao chini ya usimamizi huu? Toa maoni yako hapa chini👇👇👇!"

Comments
Post a Comment
Maoni yako ni muhimu kwetu! Unafikiri nini kuhusu mchezo au tetesi hii ya leo? Shusha mchango wako hapa chini. Kumbuka: Lugha ya staha na heshima kwa wadau wote wa soka inazingatiwa.