Mashati ndani, Mzee wa kucheka na nyavu: Ni nini sababu ya Yanga sc kumsajili Peter Shalulile kwenye klabu hiyo.
Ule usajili uliokuwa ukisubiliwa kwa hamu na mashabiki wa Yanga SC pamoja na barani Afrika kwa ujumla, Yanga SC imemtambulisha Raia wa Namibia, Peter Shalulile usiku wa kuamkia leo baada ya kuinasa saini ya mchezaji huyo baada ya kuwa mchezaji huru, Utambulisho huu umewashitukiza mashabiki wengi wa soka.
Peter Shalulile amejiunga na wanajangwani, Yanga SC kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kuachana na miamba wa soka wa kimataifa wa Afrika Kusini,Mamelodi Sundowns. Mzee wa kuchomekea alikuwa huru alipomalizana na timu yake ya zamani Mamelodi na kuwa huru , akashawishika na soka la bongo NBC Premier League, Shalulile mwenye umri wa miaka 32 mwenyi kiwango cha hali ya juu sasa hivi ni mali ya yanga.
Ujio huu kwa timu ya Yanga sc inatarajia kuwa na mwendelezo mzuri wa mashindano ya ndani na ya kimataifa. Peter Shalulile ni mchezaji mwenye hazi ya kimataifa amefanya makubwa kwenye mashindano ya Afrika Kusini na kuisaidia timu yake ya Mamelodi Sundowns kutwaa ubingwa mara kibao na kuwa mfungaji bora wa mda wote wa ligi ya Kusini kwa kufunga magoli zaidi ya 100.
Maswali yapo kwa mashabiki wengi wa soka kuwa usajili huu mzito wa Yanga sc kwa msimu huu kuna timu yoyote ya ligi kuu kama Simba sc na Azam Fc italeta ushindani wowote au kombe linarudi tena kwa wanajangwani, Yanga sc ?.

Comments
Post a Comment
Maoni yako ni muhimu kwetu! Unafikiri nini kuhusu mchezo au tetesi hii ya leo? Shusha mchango wako hapa chini. Kumbuka: Lugha ya staha na heshima kwa wadau wote wa soka inazingatiwa.