KYLIAN MBAPPÉ AFUNGUKA: "Wanaosema Ronaldo Hana Kipaji na Messi Hafanyi Kazi Ngumu Hawajui Mpira"

Mshambuliaji nyota wa kimataifa, Kylian Mbappé, amewatolea uvivu mashabiki na wachambuzi wa soka wanaolinganisha mafanikio ya Lionel Messi na Cristiano Ronaldo kwa mtazamo hasi.

<: 0.2="" 0="" 0px="" 100="" 4px="" 6px="" black="" box-shadow:="" color:="" display:="" font-family:="" gadget="" inline-block="" quot="" rgba="" rial="" scale="" transform:="" white="">


Akijibu swali kwenye mahojiano maalum kuhusu nani bora kati yake, Erling Haaland, Harry Kane, na Lionel Messi, Mbappé aliamua kuweka wazi ukweli kuhusu magwiji hao wawili wa soka duniani.

Mbappé amepinga vikali dhana ya muda mrefu inayodai kuwa Cristiano Ronaldo amefanikiwa kwa sababu ya kufanya kazi kwa juhudi tu bila kuwa na kipaji, na kwamba Messi anategemea kipaji pekee bila kufanya kazi ngumu.

Kauli ya Mbappé:"Kama unaweza kuniangalia machoni na kuniambia kuwa Cristiano hana kipaji au Messi hajawahi kufanya kazi ngumu, basi wewe hujawahi kabisa kucheza mpira (kuvaa viatu vya soka) maishani mwako."

🇫🇷Mfaransa huyo alieleza kuwa ili mchezaji afike kiwango cha juu na kukaa hapo kwa miaka mingi kama walivyofanya Messi na Ronaldo, lazima uwe na mchanganyiko wa kipaji kikubwa sana pamoja na nidhamu ya kufanya kazi kwa juhudi kila siku.


Je unakubaliana na kauli hii ya Kylian Mbappé kuhusu LIONEL MESSI na CRISTIANO RONALDO ? Weka maoni yako hapo chini👇👇 

KUTAZAMA VIDEO YA TUKIO HILI BONYEZA HAPA 

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA ALPHONCE MSANGA (MABULA) YA SOKA: Kutoka kwenye maisha ya mtaani hadi kuwa mchezaji bora wa kimataifa

Wasifu wa Albert Kangwanda Jr: Nyota Mpya wa Kimataifa Anayetamba Ndani ya Kikosi cha Yanga SC

Wachezaji bora kwenye ligi kuu ya NBC Premier League

RIPOTI KUTOKA KAMBINI: Uchambuzi wa Kikosi cha Taifa Stars na Silaha Mpya Kuelekea AFCON 2027

Fabrizio Romano Aitambulisha Yanga Duniani, Bodi ya Ligi Yaibeba Simba SC!

Rungu la TPLB: Maafisa wa Singida Black Stars Watandikwa Faini ya Tsh Milioni 20!

Mtanange wa Ligi Kuu ya NBC: Uchambuzi wa Kina wa Mechi za Kukata na Shoka Kesho

Mwelekeo wa Ligi Kuu ya NBC: Rejesho la Aziz Ki, Changamoto ya Majeraha Simba SC na Shinikizo Ndani ya Azam FC

WASIFU KAMILI: Fahamu Nguvu na Udhaifu wa Gaborone United, Wapinzani wa Yanga SC Ligi ya Mabingwa Afrika!

Ratiba Kamili na Utabiri wa Kimbinu wa Michezo ya Ufunguzi Ligi Kuu ya NBC Wikiendi Hii.