Wananchi mmeamua kuchafua hali ya hewa kabisa msimu huu! Yale mambo ya wapinzani kupeta na kupumua katikati ya uwanja sasa hivi yanaenda kuwa historia. Uongozi wa Yanga hautaki ujinga kabisa safari hii; wameingia anga za mbali kule nchini Morocco na kumlamba kiasi cha dola laki mbili na nusu ($250,000) matajiri wa Olympique de Safi ili kuipata saini ya huyu mwamba. Mkataba wa miaka miwili ushagongwa muhuri, kila kitu kipo 'done deal'. Hapa mjini kimebaki kitu kimoja tu: kile ki-video cha utambulisho cha Admin wa Yanga SC kishuke kwenye kurasa zao ili watu wazime simu zao kwa wivu!

Huyu mzaliwa wa Congo Brazzaville sio yule mchezaji wa kubahatisha au wa kuja kujaribu maisha Bongo.
Fred Duval Ngoma ni fundi wa mpira, kazi yake kubwa ni mbili tu: kwanza ni kukata umeme, kuzima mitambo ya maadui na kuhakikisha lango la nyuma haliguswi. Pili, akishapokonya mpira anaanza kugawa pasi za upasuaji kama anatumia rimoti kontroli. Ana uzoefu mkubwa wa michuano ya CAF na
alikiwasha sana msimu uliopita kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.
Pale katikati sasa hivi panenda kuwa pachungu kwa timu pinzani. Ngoma akianza kupiga midundiko yake ya kikongo, viungo wa timu nyingine watatafuta pa kutokea au wataomba mabadiliko wenyewe. Ni mtu katili wa mpira anayetia adabu.
Yanga wamemleta huyu chuma ili kuongeza uimara zaidi na kuwapa mashabiki burudani ya maana. Wananchi, hebu tokeni mafichoni, mpo tayari kumpokea huyu kiumbe anayeenda kutetemesha ardhi ya klabu ya wananchi? ๐ข๐ก๐ช
Comments
Post a Comment
Maoni yako ni muhimu kwetu! Unafikiri nini kuhusu mchezo au tetesi hii ya leo? Shusha mchango wako hapa chini. Kumbuka: Lugha ya staha na heshima kwa wadau wote wa soka inazingatiwa.